Our Blog

ISAIAH 60:1

" Arise, shine; For the light has come! And the glory of the Lord is risen upon you."

Thursday, 24 June 2021 21:07

MWANAO NAKUANDIKIA by FAITH WERU Featured

Written by
Rate this item
(4 votes)

Nimeshindwa kuzuia, leo kukuandikia
Yale umenitendea, nikiwaza ninalia
Amani umenipea, siwezi kuelezea
Mungu ninapokuwaza, ninakutabasamia

 

Umekuwa Imanueli, ni Mungu pamoja nami
Daima wewe mkweli, uongo katu husemi
Na katika zote hali, kunibariki hukomi
Mungu ninapokuwaza, ninakutabasamia

Wewe ni muaminifu, kwa kila unachosema
Meniondolea hofu, na ukanitenda mema
Sijapata hitilafu, kwangu Umekuwa mwema
Mungu ninapokuwaza, ninakutabasamia

Mwanao ninakupenda, nami nitakuishia
Kote nitakapoenda, sifa nitakupatia
Mimi kamwe sitapenda, utukufu kuchukua
Mungu ninapokuwaza, ninakutabasamia

Maneno hayatatosha, wewe kukuandikia
Machozi hayataisha, kwa vile mefurahia
Ewe Mungu menikosha, mimi ninakuinua
Mungu ninapokuwaza, ninakutabasamia
kutoka kwa bintio :Mchele wa chenga

Read 769 times Last modified on Sunday, 10 April 2022 12:23
More in this category: « Restoration. TOTAL SURRENDER »

Leave a comment

Make sure you enter all the required information, indicated by an asterisk (*). HTML code is not allowed.

Slider