TUENEZENI AMANI
UONGOZI SIO CHAMA
Ya mgambo imelia, hodihodi naingia
Sina kinyongo kabisaa, nimekuja kwa uzuri
Ule muda umewadia, ya kura kuwapigia
Uongozi sio chama, wa kukufaa chagua
Waziwazi nitasema, hili sitanyamazia,
Siku hiyo raukia, wa manufaa chagua
Lisa Ni kulirudia, pale tulipokosea
Uongozi sio chama, wa kukufaa chagua
Miaka na mikaka, tumeumia kwa Hilo
Kweli tumeambulia, kwa wasiotusaidia
Magari wanatembelea, maskini tukiumia
Uongozi sio chama, wa kukufaa chagua
Ahadi za kutuhadaa, hela kutumwagia
Halafu tuhadaike, kura tutawapigia
Mitini wataingia, yetu watapuuza
Uongozi sio chama, wa kukufaa chagua
Beti tano nakomea, wosia kuwapatia
Hekima nimewagawia, ili msije jutia
Kwa makini zingatia, time kupiga hatua
Uongozi sio chama, wa kukufaa chagua